Theluji yaathiri maisha kwa kiasi kikubwa nchini Ujerumani

Kwa sababu ya theluji nzito katika uwanja wa ndege wa Cologne-Bonn, imeripotiwa kuwa baadhi ya safari za ndege zimeahirishwa tangu saa 09.15 asubuhi na ndege nyingi zimechelewa.

Katika miji mingine, hasa  Kaskazini Rhine-Westphalia (KRV), treni za kasi hazikuweza kufanya kazi.

Kutokana na theluji ikimbatana na mvua kubwa, magari yameshindwa kutembea barabarani na ajali nyingi kutokea.

Shirikisho la Hali ya Hewa la Ujerumani limetangaza kwamba hali ya hewa itaendelea kwa siku kadhaa.

Wataalamu wametoa onyo kwa magari na watembea kwa miguu hasa dhidi ya ajali zinazosababishwa na barafu nyingi.
Mpya zaidi Nzee zaidi