Yanga SC walia na ratiba ya Ligi


Yanga SC wataka kuwepo kwa namna bora zaidi ya upangaji ratiba ya Ligi kwani wachezaji wanatumia muda mwingi kusafiri kitu kinachoweza kuathiri matokeo yao uwanjani.

Msemaji wa Yanga SC, Dismas Ten amesema kuwa wachezaji wanatumia muda mwingi kusafiri na kupata muda mchache wa kupumzika.

"Masaa 72 ambayo timu inabidi ipumzike,  yanamalizika timu inaingia Uwanjani na mazingira yetu ya usafiri jinsi yalivyo si rafiki kwani wachezaji wanatumia muda wa kumpumzika wakiwa safarin," amesema.

Hadi sasa Yanga SC inaongoza Ligi Kuu Soka Tanzania (TPL) ikiwa na pointi 53 kibindoni na wakiwa wamecheza michezo 20, huku wapinzani wao wa jadi, Simba SC wakishika nafasi ya nne na pointi 33 lakini wakiwa wamecheza michezo 14 pekee.
Mpya zaidi Nzee zaidi