CUF yatangaza kujitoa UKAWA


Katibu Mkuu mpya wa Chama Cha Wananchi CUF, Khalifa Suleiman Khalifa, amesema wao kama chama cha Wananchi wameshajitoa kwenye mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi 'UKAWA' kwa madai upo hoi na hauna msaada kwao

Khalifa amesema kwamba, msimamo wa CUF ni kutoshirikiana na UKAWA kwasababu wabunge wa CHADEMA na wafuasi wake wameshindwa kuwa na ushirikiano katika matatizo waliyokuwa nayo

Ameongeza kwamba kwa muda mrefu Wabunge wa CHADEMA wamekuwa wasemaji waliokuwa wakimuunga mkono, aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Maalim Seif Sharif

Umoja wa Katiba ya Wananchi, (UKAWA) uliundwa na vyama vya NCCR-Mageuzi, NLD, CUF na CHADEMA ambapo baadaye waliungana katika uchaguzi mkuu wa 2015