Rais Magufuli awaita Taifa Stars, viongozi wa TFF leo Ikulu


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo atakutana na wachezaji wa wa Taifa Stars, Viongozi wa TFF, Kamati ya Uhamasishaji na Bondia Hassan Mwakinyo Ikulu Dar Es Salaam.

Katika  kukutana nao atawapongeza na kula nao chakula cha mchana.

"Mhe. Rais Magufuli leo Machi 25, 2019 atakutana na wachezaji wa Taifa Stars, Viongozi wa TFF, Kamati ya Uhamasishaji na Bondia Hassan Mwakinyo Ikulu DSM. Atawapongeza na kula nao chakula cha mchana. Tukio litarushwa Live! na Redio, Televisheni na Mitandao kuanzia saa 4:00 asubuhi," ameandika Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa kwenye ukurasa wake wa Twitter.