Kauli ya Serikali kuhusu ujenzi wa barabara za ndani


Na Thabit Hamidu,Zanzibar.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ),imesema  haina mpango wa kuunda sheria itakayozipa mamlaka  Serikali za mitaa uwezo wa kutengewa fungu la  kusaidia kukamilisha shughuli za ujenzi wa  barabara za ndani.

Kauli hiyo ameitoa jana Naibu waziri wa Nchi Ofisi Ofisi ya Raisi ,Tawala  za mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalumu za  SMZ Shamata Shaame wakati akijibu swali la Hidaya  Ali Makame ambaye ni Mwakilishi wa nafasi za  wanawake ambapo alitaka kujua mpango wa serikali  katika kuzipa mamlaka hizo za kutengewa fungu la fedha.

Akijibu swali hilo alisema serikali haitaandaa  sheria hiyo badala yake itaendelea na utaratibu  wake kutoa fursa kwa Halmashauri za Wilaya kupata  ruzuku kutoka serikali kwa ajili ya utekelezaji wa mipango yake ikiwemo matengenezo ya barabara za ndani.

Naibu Waziri huyo alisema uwezo wa kutenga fungu hilo utaweza  kutekelezwa iwapo fedha zinazotolewa na mfuko wa  Barabara zitaengezeka kutoka asilimia 15 inayotolewa sasa hadi kufikia asilimia 40 ya  bajeti ya matengenezo ya barabara za ndani  hususan vijijini.

Alisema ni kweli kuwa Halmashauri za wilaya  zimekuwa vinakabiliwa na tatizo kubwa la  matengenezo ya barabara za ndani jambo ambalo  linakosesha fursa ya kuzifikia Barabara zote  zinazohitaji kutengenezwa.

"Ninachukua fursa hii kuzishauri Halmashauri kudhibiti vyanzo vya mapato ya ndani ili pamoja na kuongeza kasi ya ukusanyaji wa  mapato ili fedha zitakazo patikana ziweze kukidhi mahitaji yaliyokusudiwa,"alisema Naibu Waziri huyo.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia