Azam FC yamsajili winga wa Mbeya City

Idd Seleman 'Nado',amesajiliwa na Azam FC kwa kandarasi ya miaka miwili akitokea  Mbeya City.

Nado amesaini mkataba huo mbele ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim Amin 'Popat' na Mratibu wa timu, Phillip Alando.

Nado akiwa Mbeya City alitupia kambani jumla ya mabao 10 msimu uliopita, ni sehemu ya mapendekezo ya Kocha Mkuu mpya wa Azam FC, Etienne Ndayiragije.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia