Marekani na Uingereza walaani shambulizi lililowalenga wanadiplomasia wa Uturuki

Wanadiplomasia wa  Uturuki wameshambuliwa   mkoani Erbil nchini Iran na watu waliokuwa na silaha.

Shambulizi hilo limelaaniwa  na mataifa tofauti ikiwemo pia Uingereza na Marekani.

Shambulizi hilo liliwalenga wanadiplomasia wa Uturuki katika mgahawa mmoja  Jumatano na kupelekea mmoja miongoni mwa wanadiplomasia hayo kufariki.

Mwili wake umewasili Uturuki kwa ajili ya mazishi.

Baada ya shambulizi, mwili wa mwanadiplomasia aliefariki  ulipelekwa katika hospitali ya  Rizgari kwa  ajili ya uchunguzi.

Muakilishi wa Uingereza Umoja wa Ulaya  na Marekani Alan Duncan amelaani tukio hilo kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Uingereza imetoa mkono wa pole kwa Uturuki kufuatia maafa ya  mwanadiplomasia wake nchini Irak.

Mike Pompeo pia amekemea shambulizi hilo.