Chelsea ya Lampard kukipiga Darajani kwa mara ya kwanza leo

Klabu ya Chelsea leo itacheza mchezo wake wa pili wa Ligi Kuu England dhidi ya Leicester City.

Mchezo huu utakuwa ni wa kwanza kuwa nyumbani baada ya ule wa kwanza kupoteza ugenini kwa kufungwa mabao 4-0 mbele ya Manchester United.

Frank Lampard, Meneja wa Chelsea amesema kuwa utakuwa mchezo mgumu na wenye ushindani mkubwa.

Mchezo huu utachezwa uwanja wa Stamford Bridge.