Mashine ya Utra Sound yaibwa Hospitalini


Mashine ya Utra Sound imeibiwa katika mazingira ya kutatanisha ndani ya wodi ya wazazi katika Hospitali ya mji wa Bariadi.

Mashine hiyo ilipotea tangu Agosti 5 mwaka huu mchana na hadi sasa watumishi 17 wa hospitali hiyo wamefikishwa polisi kwa mahojiano zaidi.