Mbunge Sugu aoa, Wabunge wa Chadema wamiminika


Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) leo Jumamosi Agosti 31, 2019  amefunga ndoa takatifu na Mke wake, Happiness Msonga ambaye hivi karibuni walibahatika kupata mtoto mmoja.


Sugu na mkewe huyo wamefunga ndoa katika Kanisa Katoliki Ruanda Parokia ya Roho Mtakatifu lililopo jijini Mbeya.

Wabunge waliohudhuria ni pamoja na Anthony Komu , Lucia Mlowe, Sophia Mwakagenda na Lucy Mollel (wote Viti Maalum) Frank Mwakajoka (Tunduma), Joseph Haule (Prof. Jay), Joseph Selasini , David Silinde (Momba), Pascal Haonga (Mbozi) na Wilfred Lwakatare (Bukoba  Mjini).

Mbunge wa Jimbo la Mikumi, Proffesor Jay ameandika "Hongereni sana kaka yangu @jongwe__ na Shemeji yetu Happiness msonga kwa kukamilisha ndoa yenu takatifu Leo, Tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu Awabariki zaidi na awasiamie kwenye Maisha yenu ya NDOA, AMEN."