Mchezaji ajirekodi akifanya ngono na kuirusha video mtandaoni


Winga wa zamani wa Tottenham na Raia wa Cameroon, Clinton N’Jie alijikuta akitazamwa na mamilioni wa watu ulimwenguni akifanya ngono, baada ya kutuma video yake kimakosa mtandaoni.

Mchezaji huyu alikuwa akifanya ngono lakini ghafla akabonyeza kitufe tofauti ambacho kilisababisha arushe mubashara tukio lake hilo kwenye mtandao wa SnapChat.

Hata hivyo, baada ya kufuta video hiyo ambayo tayari ilikuwa imeshatazamwa, N’Jie aliomba radhi akisema alikuwa amelewa sana kutokana na furaha aliyokuwa nayo baada ya kusaini mkataba wa miaka minne na Klabu ya Dynamo Moscow ya Urusi akitokea Olympique Marseille ya Ufaransa.

Baada ya kusaini mkataba huo, inadaiwa kuwa N’Jie alitaka kuingia kwenye Google ili aisome habari yake lakini akajikuta akibonyeza kitufe kingine kimamosa kilichosababisha arushe ‘live’ tukio lake akifanya ngono na mwanamke mmoja aliyekuwa amesuka nywele.