Mchezaji wa Zamani 'amwaga misaada' Yanga SC


Mlinzi wa zamani wa Yanga SC, Ahmed Amasha, leo ameukabidhi uongozi wa timu hiyo vifaa mbalimbali vya mazoezi

Amasha aliyeitumikia Yanga SC kati ya mwaka 1980 na 1985, amekuwa na utaratibu wa kutoa misaada mbalimbali kwa klabu hiyo

Amasha kwa sasa anaishi Arabuni, amewataka wadau wengine wa Yanga SC ambao wanaishi nje ya nchi wasiisahau timu yao.