Mwenyekiti CCM aridhishwa na miradi ya maendeleo


Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Mtwara Yusuph Nnanila, ameonyesha kuridhishwa na usimamizi wa miradi katika Manispaa ya Mtwara Mikindani ambapo amewataka watumishi wa halmashauri hiyo kuendelea kutekeleza miradi hiyo kwa kasi ili kuweza kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano.

Akizungumza wakati wa ziara ya kamati ya siasa ya Mkoa huo katika ukaguzi wa miradi ya maendeleo amesema kuwa usimamizi huo umekuwa wa hali ya juu na ameridhishwa na ujenzi wa soko la kisasa, ujenzi wa barabara ambao unaenda kwa kasi inayotakiwa.

“Ni kweli naona manisapaa wanajitahidi sana kufanyakazi na kuwa na usimamizi mzuri ambao unaanzia kwenye soko kubwa la chuno na kituo cha mabasi cha mikindani, ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami usimamizi huu uendelee ili kuweza kuendana na kasi ya Rais John Magufuli,” amesema Nnanila.