Jumuiya ya wanawake ya chama cha CUF (JUKE CUF) Jumamosi hii katika ukumbi wa hoteli ya Mtanzania uliopo Tandale jijini Dar es Salaam, semina kwa wanawake kutumia fursa ya kushiriki kugombea nafasi mbali mbali kwenye chaguzi zinazokuja ikiwemo serikali za mtaa Novemba 24 mwaka huu.
Semina hiyo imehudhuriwa na mgeni rasmi sambaye ni katibu mkuu wa CUF taifa, Khalifa Suleiman, mwenyekiti wa JUKE CUF Kiza Mayeye (Mbunge viti maalum Kigoma), Sonia Magogo (Mbunge viti maalum Tanga), Anna Lioba (Katibu Juke CUF).


