Jinsi ya kumchangamsha na kumfurahisha mwanamke


Kila mwanaume anapenda kujua jinsi ya kumchangamsha mwanamke ili ampende. Lakini wengi hushindwa njiani pale wanapojaribu kufanya hivyo kwa sababu hawajui vitu vitano vya kumchangamsha mwanamke.

Yafahamu hayo mambo matano, na namna kuyatumia.

Nadhani utakuwa ushashuhudia baadhi ya wanaume wakichati na wanawake(zao),wakati mwingi unakuta mwanamke anacheka na kumsifia kuwa anamfurahisha(“hahahaha!…. unanifurahisha”).

Kuambiwa na msichana kuwa unamfurahisha ni mojawapo ya kitu kikubwa sana ambacho wanaume wengi hawakisikii kutoka kwa mwanamke. Haihusiani na muonekano wako, ila namna unavyopangilia hoja zako na mada zako kwake na jinsi unavyoziwasilisha kwa kuangalia mazingira.

Jinsi ya kumfurahisha na kumchangamsha mwanamke
Ni kitu gani hasa kinamfurahisha mwanamke? Hauwezi kumfurahisha mwanamke kwa kumkejeli au kumshika baadhi ya maeneo ya mwili wake(utaishia kumchukiza na kujiondolea point).

Utajua unamfurahisha mwanamke pale tu unapomfanya ajisikie furaha, na wakati mwingine hushindwa kujizuia na hujikuta anakukiss!.

Ntakupa mambo matano ya kufanya ambayo yakuufurahisha moyo wa msichana unayemtaka(kumpenda).

Unaweza kubadilisha muonekano wako kimavazi, wakati mwingine unaweza kumkazia macho lakini hiyo haitamfurahisha bali itamtisha.

Kumchangamsha/kumfurahisha mwanamke kunahitaji kutengeneza mvuto(impression) zaidi ya muonekano na swaga.

Kama unataka kujua jinsi ya kumfurahisha mwanamke , mwanzo wa yote, huanza na maongezi. Na mwisho wa yote ni hapo pia.

Mawasiliano mazuri kimaongezi ndiyo njia pekee ya kumfurahisha na kumchangamsha msichana.

Yatumie haya mambo matano, na utafanikiwa hata kabla ya kufikia mwihso:

1. Mshawishi kupitia kitu anachokipenda
Unaweza kudahani hii haina umuhimu. Wanaume wengi hufikiri hivyo na hushangaa kwanini tu niongee kuhusu kitu ambacho msichana anakipenda. Kwanini wasichana nao wasiongee kuhusu vitu wanavyovipenda wanaume?

Wanawake huweza kufanya hivyo, japo hatujui. Wanawake wengi hujitahidi sana kujua wavulana hupenda kuongelea nini. Lakini, wakati unataka kumvutia msichana, ni muhimu ukajua ni kitu gani kinachoendelea kwenye mawazo yake. Sasa tambua kwamba, kujua kitu msichana anachokipenda haimaanishi, dhahabu, mitindo au vipodozi. Tofauti kati ya msichana na mvulana kwa namna ya kuishi imepungua sana kwa sasa(wanawake hufanya vingi ambavyo wanaume hufanya). Kwa maana hiyo ni rahisi kuwa na maongezi yenye kuvutia bila kuboa. Achana na mambo ya mahesabu, michezo, teknolojia, amini yatakua poa tu maongezi yenu.

2. Mtanie
Unapoongea na msichana, ni rahisi sana kumfanya na yeye aongee na wewe hatakama hakupenda mwanzo. Lakini hiyo haitoshi. Kama unataka kujua ni jisi gani ya kuongea na msichana/mwanamke, utapaswa kumfanya yeye ajisikie huru na mwenye kujiamini(confortable), lakini pia mfanye ajue kuwa unampenda hatakama haujamwambia.

Kumbuka, kama utaongea nae kama rafiki, lazima awaze na ajue kuwa wewe ni mwanaume noma sana(great guy), lakini hatahisi kwamba wewe ni mwanaume unaeweza kumchangamsha au kumfurahisha. Ili kuonekana kama mwanaume anayefurahisha kwa mwanamke yeyote, inatakiwa akuone kama mtu muhimu wa kukutana nae, na ili kufanya hivyo, msukume sukume hata bega katikati ya maongezi. Lakini usizidishe sana utaishia kumboa, fanya hivyo pale tu anapoongea jambo linalochekesha au lenye utani ndani yake.

Ila usiende na kumwambia maneno ya kawaida kama “unamuonekano mzuri”, “wewe ni mzuri sana”, au maneno yenye kufanana na hayo. Inawakera sana na haioneshi utofauti na watu wengine wa mtaani. Badala yake, jaribu kuwa specific wakati unamuambia jambo fulani mnapokutana. Mwambie maneno kama “umependeza sana leo. Huo ni mtindo mpya wa nywele?”, Hayo ni maneno mazuri sana kwa mwanamke kwa sababu ni wanaume wachache sana huyatumia kwao. Kwa hiyo unavyosema “leo umekua mrembo zaidi” inamfanya ajue ni jinsi gani unamaanisha mpaka umevunja ukimya.

Kwa kumtania huko – unaweza kufanya mambo matatu. Unaweza kumshtua na kumfanya atabasamu. Unaweza kumfanya ajue kwamba wewe unamuona mtu wa tofauti sana. Au tatu, unaweza kumfanya atambue kwamba umemwona wa kuvutia sana. Kumbuka hayo yote unamfanya yeye aone ni mtu mzuri ambaye anaweza kudate na wewe.

3. Kuwa mcheshi(be funny).
Baada ya kumfanya atabasamu na kuyafurahia maongezi yako na yeye, ni muda wa kumuingia ndani zaidi kidogo. Kila mmoja wetu anamambo yake ya siri ambayo hatupendi watu wote wajue labda mtu ambaye tunamwamini sana. Ili kumfanya ajiamini kwako, unatakiwa kumfanya awe na good time sana na wewe. Sasa hatuwezi kukuambia kabisa jinsi ya kumfanya mwanamke acheke. Lakini tunaweza kukupa mambo mawili ya kutumia. Usimwambie utani wowote wakati unaongea nae. Kuwa mwenye furaha muda wote unaoongea nae.

Hii inaweza kukutatiza kidogo. Kwanza kuongea utani wa moja kwa moja kama mtu aliyekariri ni ujinga. Badala yake, ongea nae maongezi yatakayomfanya aone unamtania, na hapo naye ataanza utani.

Jitahidi kuonesha unafurahia maongezi wakati unaongea nae kama unataka kumchangamsha. Ukiwa na furaha, dunia nzima inatabasamu pamoja nawe!. Kama unatabasamu na kujisikia furaha, naye atatabasamu pia na kuwa na furaha. Lakini kama unauoga, utamfanya naye awe
mwoga(unconfortable).

4. Unaweza kumsukuma kidogo kati kati ya maongezi
Najua unaelewa ninaposema kusukumana, hii utokea mara nyingi pale mvulana na msichana wanapukua wamezoeana, kwa hiyo kuifanya na mwanamke kwa mara ya kwanza inatakiwa uwe mwangalifu na makini ili usije kuharibu. Unapofanikiwa kufanya hivyo, jitahidi isiwe kila saa maana utamkera kama nilivyosema hapo awali.

Ili uweze kufanya hivyo inatakiwa uwe wa kawaida – chukulia kama ni mtu wa kawaida japo wewe unajua ni special. Muulize alifanya nini weekend au baada ya kutoka kazini, muulize anapenda kwenda wapi akitoka out au ni mgahawa gani anaupenda au anatamani kwenda au kitu kingine chochote ambacho ni binafsi(very personal). Lazima atajua wewe unamtania mana hakuna mtu ambaye anaweza kuulizwa maswali yote hayo na hajazoea kuulizwa, hivyo lazima afunguke.
Na bila kusitaa, usisahau kuuliza hili swali.

“Hey, samahani hii ni very personal – hivi una boyfriend? Kama unaye basi jua moyo wangu utavunjika vipisivipisi zaidi ya millioni hamsini sasa hivi!”, umeona ilivyo ya kichokozi eeh?. Lakini hii hufanya maajabu!.

Lazima acheke, lakini hiyo sentensi itaweka lengo lako kwake moja kwa moja, na lazima atajua kuwa unamtaka–hahahah!. Lakini angalia usiharibu kwa kuwa kituko baada ya kukupa jibu – maana unaweza kuta anaye, na kama atakwambia anaye tabasamu. Na ongelea mada nyingine tofauti kama vile swali lililopita halikumaanisha kitu kwako. Lengo lake lazima atakuwa ashalijua, na pia utafanikiwa kumfanya awe confortable kwako.

5. Mshike.
Huu ni uwanja hatari sana, lakini ni kitu unachopaswa kujifunza kwa sababu unataka kujua jinsi ya kumchangamsha msichana, si ndiyo? Hivyo kumshika katika muda muafaka inakamilisha point ya 5 ya mambo ambayo unapaswa kuyajua wakati unataka kumfurahisha mwanamke. Kama utafanikiwa kulifanya hili kwa usahihi, utakua umejichukulia point kubwa sana.

Sasa kumshika msichana ni kama kucheza na moto. Ukiushika fasta hauwezi kusikia joto, lakini ukiushika muda mrefu utaungua! Unaona ilivyo hatari?
Unaweza kumshika bega au mikono kama tayari ushamfurahisha vya kutosha. Lakini kumbuka hili, mshike tu pale unapokua na sababu ya kumshika, mfano mshike masikio kama unayasifia masikio yake au nywele kama unazisifia nywele zake, au mfute koti lake kama kuna kauchafu hatakama hana hako kauchafu, au mshike begani kama unatembea nae barabarani/ mtaani. Kumbuka kumshika mtu ni very personal, hivyo inabidi uwe makini sana na uangalie anamuitikio gani wakati unamshika kabla haujamshika tena.

Kama unataka kujua jinsi ya kumchangamsha msichana, yatumie haya mambo matano wakati utakapokutana na mwanamke next time. Na baada ya hapo utaona ni jinsi gani unavyoweza kumfurahisha mwanamke na kumfanya ayapende maongezi yako kwa mara ya kwanza!.