PICHA: IGP Sirro akiwa Zanzibar

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akipokea salamu ya heshima wakati alipowasili visiwani Zanzibar leo kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja kwalengo la kukagua miradi ya ujenzi wa nyumba za askari pamoja na kuzungumza na maofisa na askari wa vyeo mbalimbali. Picha na Jeshi la Polisi.


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, akipita kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba za askari Polisi zilizopo katika eneo la Fuoni wakati alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja leo Kisiwani Zanzibar na kuzungumza na maofisa na askari wa vyeo mbalimbali. Picha na Jeshi la Polisi.