https://monetag.com/?ref_id=TTIb Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa Usalama wa Taifa afariki dunia | Muungwana BLOG

Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa Usalama wa Taifa afariki dunia


Mkurugenzi mkuu mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa (Tiss), Apson Mwang’onda (75) amefariki dunia jana nchini Afrika Kusini.

Taarifa za familia yake zinaeleza kuwa Mwang’onda alikuwa akisumbuliwa na saratani alilazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na baadaye kuhamishiwa Afrika Kusini.

Mwang’onda alikuwa mkurugenzi wa idara hiyo kuanzia mwaka 1995 hadi 2005, akiwa mkurugenzi wa sita wa idara hiyo tangu mwaka 1961.