Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 5.2 laikumba China

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 5.2 limetokea katika Mkoa wa Guangsi Zhuang kwenye mpaka na Vietnam kusini mwa Uchina.

Kituo cha Mtandao wa matetemeko ya ardhi cha China (CENC) kimesema katika taarifa kwamba tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 5.2 limerikodiwa kutokea majira ya saa 09.18 Jingxi, Mkoa wa Guangxi Zhuang.

Kwa mujibu wa habari,tetemeko hilo limefikia kina cha kilomita 10 kaskazini mashariki wa Vietnam.

Hakuna aliyepoteza maisha katika tetemeko la hilo.
Mpya zaidi Nzee zaidi