BREAKING NEWS: Rais Magufuli asamehe Wafungwa 5533


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametangaza kusamehe Wafungwa 5533 huku akisema kuwa Mkoa ambao wafungwa wengi wameachiwa ni Mkoa wa Kagera 713 wakifuatiwa na Mkoa wa Dodoma.

Rais Magufuli ametoa leo wakati wa kusherekea Miaka 58 ya Uhuru wa Tanzania Bara inayofanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

"Kwa kutambua kuwa hakuna binadamu mkamilifu, na Mungu sisi anatusamehe kila siku. Leo Novemba 9, 2019 nimeamua katika kusherehekea miaka 58 nimeamua kusamehe wafungwa 5533 najua ni idadi kubwa watu watashangaa, lakini nimeamua kutumia Siku hii ya Uhuru kusamehe maana sifurahi kuongoza Nchi yenye Watu wengi Magerezani ," amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli amesema“Nilipotembelea Gereza la Butimba niliumia sana kukuta Wafungwa kule wengine kesi zao za kubambikiwa na najua hii iko Nchi nzima, mwingine amefungwa kisa tu aligombana kidogo na Mpenzi wake au Mshikaji wake."
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia