Waziri Zungu apiga stop nguo za ndani za mitumba


Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mussa Zungu amepiga marufuku nguo za mitumba za ndani  kwakuwa zinasababisha maradhi kwa watumiaji.

"Nguo za mitumba ambazo haziruhusiwi ni nguo za ndani kwa sababu ya maradhi, mfano Mwanamke anavaa vazi la juu (sidiria) huwezi kujua aliyevaa kabla yako alikuwa ana magonjwa gani, huo ndio mwanzo wa kusambaa kwa magonjwa ya saratani"

“Nimefanya ziara Mto Msimbazi shughuli za Binadamu zinaharibu kingo za Mto, Kuna mazungumzo yanaendelea kati ya Serikali na Benki ya Dunia ya ujenzi wa Mto Msimbazi, na tunatarajia kujenga Barabara ya juu kutoka Magomeni Mapipa hadi Faya na maji yatapita chini"-Zungu