Bondia Wilhelm Ott kutoka Australia abadili dini na kuwa muislamu


Bongia mashuhuri nchini Australia Wilhelm Ott   abadili dini na kuwa muislamu baada ya kuvutiwa na mwenendo wa rafki yake mturuki.

Wilhelm Ott  , bondia nchini Australia abadili dini na kuwa muislamu  baada ya  kuvutiwa na mwenendo wa rafiki yake mturuki .

Bondia huyo ameonekana katika video akitoa shahada,  ishara kuwa anakubali na kuamini uislamu  amesema kuwa anamshukuru Allah kumonesha imani ya haki.

Wilhelm Ott   amesema kuwa kuwa muislamu ilikuwa malngo yake ila alikuwa bado hajakinahi kutokana na taarifa nyingi ambazo zilikuwa zikimchanganya kutokana na uislamu anavyozungumziwa,  ila katika kipindi cha  agizo la kutotoka ndani  kutokana na virusi vya corona  ameweza kujifunza mengi na kupata nguvu ya kuchukuwa uamuzi wa kuwa muislamu.

Wilhelm Ott   ana umri wa miaka 37.

Katika video yake hiyo, Wilhelm Ott   amesema kwamba rafiki yake mturuki  pia umemsaidia na kumpa  Quran yake ya kwanza.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items