Mwanamuziki Mory Kante afariki dunia

Mwanamuziki Mory Kante aliyetamba katika anga la muziki miaka ya 1980 amefariki dunia akiwa na miaka 70 mjini Conakry, Guinea baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Kante alivuma sana Afrika nzima na wimbo wa Yeke Yeke ambao ulivuma hadi nchi kadhaa za Ulaya.