Shambulizi la bomu nchini Somalia

Watu  10 wameuawa na wengine  13  wamejeruhiwa katika mlipuko wa bomu uliotokea nchini Somalia.

Shambulizi hilo limelenga  magari ya cuhukuzi wa umma  na kusababisha vifo vya watu  10 na  wengine zaidi ya  10 kujeruhiwa.

Kamanda wa jeshi la Polisi katika eneo la Shebelle, Hussein Abdi Ali  amewaambia wanahabari kuwa   shambulizi la bomu la kuvizia limelenga  basi moja la  uchukuzi wa umma katika eneo hilo na kusababisha maafa.

Hakuna   kundi lolote ambalo limejinasibu kuhusika na tukio hilo  huku wanamgambo wa kundi la Boko haramu wakishukiwa  kuhusika na shambulizi hilo.

Kufuatia  shambulizi hilo, jeshi la Somalia limefahamisha  limeendesha operesheni kali   katika eneo hilo na kuwaangamiza wanamgambo  18 wa al Shabaab.

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia