Afrika Kusini yafanya jaribio la kwanza la chanjo ya Covid-19


Afrika Kusini imeanza jaribio la kwanza la chanjo dhidi ya virusi vya corona  barani Afrika.

Chanjo hiyo imefahamishwa kutengenezwa na kituo cha utafiti cha   Chuo Kikuu cha Oxford na tayari imeanza kufanyiwa majaribio kwa binadamu nchini Uingereza.

Nchini Afrika Kusini idadi ya watu   walioambukiwa  virusi hivyo inakaribia kufikisha watu  140,000 huku watu 2,500 wamefariki dunia na bado ni nchi iliyoathiriwa zaidi barani Afrika na janga hilo la Covid-19.

Chanjo inayoitwa ChAdOx1 nCoV-19 inatarajiwa kufanyiwa majaribio kwa watu 2000 waliojitolea nchini humo.

Vipimo vya utafiti vinaendelea nchini Uingereza kwa watu 4,000 huku  utafiti mwingine umepangwa kufanyika  nchini Brazil kwa watu 5,000.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items