Haji Manara aipongeza Yanga kwa kumtimua kocha wake " Mmechukua hatua sahihi kwa wakati"

Msemaji wa klabu ya soka ya Simba Haji Manara ametoa pongezi kubwa kwa uongozi wa yanga baada ya kufanya uamuzi wa kumtimua kocha wake.

Kauli hiyo ameitoa kwenye ukurasa wake wa instagram na kuandika hivi;

Hongereni Yanga sc kwa kuchukua hatua sahihi na kwa wakati, hamkubaguliwa peke yenu ni Watanzania wote,
Kampuni yangu ya H&M iliyopo South Africa 🤪🤪🤪ilibidi iombe radhi kwa tangazo la kibiashara lilionyesha viashiria vya kiubaguzi, vp tumuache muhuni huyu Mpiga Disco!!
Ktk hili mmepatia Washindi wa Pili wa ligi kuu.,,Shida yenu ni uwanjani tu 🤪