Ndege hizo za kampuni ya Marekani ya Zipline zilianza kufanya kazi nchini Rwanda mwaka 2016 zikisaidia kupeleka damu na dawa katika maeneo ya vijiji vilivyotengwa na maeneo mengine.
Lakini sasa zimeanza kuwahudumia wagonjwa wa saratani ambao maisha yao yangekuwa hatarini bila kumuona daktari.
‘’Wakati wa sheria ya kutotoka nje tuliona kwamba ilikuwa ngumu kwa wagonjwa kusafiri kwenda hospitalini kwa ajili ya kupata dawa za kansa kwa sababu lazima watibiwe na wataalamu’’Daktari Bigirimana Jean Bosco aliiambia BBC
Ndege za kampuni ya Zipline hufanya safari zaidi ya 20 kwa siku kusambaza dawa katika vijiji vya masharikiya Rwanda ambako ni vigumu kwa safari za gari.
‘’Ndege ikifika katika hospitali au zahanati hudondosha kifurushi cha dawa kwa njia ya kielectroniki kisha inarudi yenyewe katika kituo chake cha kupakia dawa nyingine.Hii ndiyo njia salama ambayo pia inapunguza urefu wa safari.drone hutumia dakika 45 kwa safari ya masaa 6 ya kutumia gari ‘’Blaise Musabe ni mfanyakazi wa kampuni hiyo amefafanua.
‘’Drone ilitusaidia sana kutufikishia dawa hapa nyumbani, tulipopokea sheria ya kutotoka nje kutokana na covid19 nilianza kuingiwa na wasiwasi kwamba maisha yangu yatakuwa hatarini. Awali nilikuwa natumia kama dola 30 kulipia nauli ,hapo sijataja uchovu wa safari pamoja na kuacha biashara zangu,nafurahi sana mpango huu unatusaidia’’Marie Louise Kagoyire,ni mgonjwa wa kansa ya damu.
Tangu mwezi Aprili, wagonjwa zaidi 270 wa kansa tayari wamesaidiwa kwa kufikishiwa dawa na drone .
