China na Marekani wavutana mbele ya mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa


Mvutano kati ya Marekani na China ulijitokeza mbele ya mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa mjini New York, baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kuilaumu China kwa kueneza virusi vya corona.

Alitaka China "iwajibishwe" kutokana na janga la corona.

Kati hotuba yake, Rais wa China Xi Jinping alisema nchi yake "haina nia ya kuingia katika Vita Baridi na nchi yoyote".

Mkutano wa mwaka huu mjini New York unaendeshwa zaidi kupitia mfumo wa kidijitali, huku viongozi wa duniani wakiwasilisha hotuba zilizorekodiwa.

Mfumo huo mpya ulimaanisha sarakasi za siasa za kimataifa zinazoshuhudiwa katika mkutano huo hazikuwepo. Kila nchi iliwakilishwa na mjumbe mmoja na kulikuwa na nafasi kidogo sana kwa nchi kujibizana.

Lakini kama ilivyotarajiwa, Rais Trump alitumia hotuba yake kushambulia mahasimu wake

Post a Comment

0 Comments