Rais Magufuli aliagiza jeshi la polisi kumuachia Mwalimu Mkuu shule waliofariki wanafunzi 10


Rais wa jamhuri ya muunganonwa Tanzania na mgombea Urais kupitia chama cha CCM ameliagiza jeshi la polisi mkoani Kagera kumuachia huru mkuu wa shule ya Byamungu Islamic iyoungua hivi karibuni na kusababisha vifo vya watoto kumi walikuwa wanasoma sshuleni hapo.

Rais Magufuli amesema kuwa mkuu wa shule hakuwa na nia ya kuanzisha shule na kuwachoma moto watoto hao na kwamba hata akiwa nje ya mahabusu bado ataendelea kushirikiana na jeshi hilo katika kubaini chanzo cha moto huo.

Aida ameitaka wizara ya elimu hapa nchini na TAMISEMI kuhakikisha wanafanya ukaguzi wa kina kwa shule zote kabla ya kufunguliwa ili kuondoa matatizo yanayoweza kutokea kutokana na matatizo ya kiufundi na miundombinu.

Post a Comment

0 Comments