Wachimbaji migodi Zambia 'waliowekwa karantini na mwajiri wao mchina waachiliwa huru'


Kundi la wachimbaji migodi raia wa Zambia walioshikiliwa na mwajiri wao Mchina kwa miezi mitano kama hatua ya kiusalama kukabliana na virusi vya corona wameachiliwa huru, kulingana na taarifa ya tovuti ya gazeti la Lusaka Times.

Kuachiliwa kwao huru Jumapili kumetokea baada ya mbunge wa eneo kuingilia kati.

Walikuwa wamekamatwa ndani ya migodi 9 kuzuia wasipate maambukizi ya virusi vya corona na kuwaambukiza wasimamizi wao raia wa China.

Makamu rais Saulos Chilima aliliambia bunge wiki mbili zilizopita kwamba serikali haikuwa na ufahamu wa kuzuiliwa kwao, ripoti ya tovuti hiyo inasema.

Inasemekana mameneja wa China waliondoka kwenye mgodi huo pale ujumbe wa maafisa wa serikali uliwasili kuwaachilia huru wachimbaji hao midogi.

Hadi kufikia sasa, Zambia imethibitisha

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items