Mwanaume moja nchini Nigeria anashutumiwa kutengeneza video ya kughushi ya Rais Muhammadu Buhari akimuoa mmoja wa mawaziri wake wa kike na kuichapisha mtandaoni ameshtakiwa katika jimbo la Kaskazini la Kano.
Video ilimuonesha Rais Buhari na Waziri wa masuala ya kibinadamu Sadiya Umar Farouq.
Kabiru Mohammed alikamatwa na mamlaka za usalama mwezi Januari lakini alishtakiwa siku ya Jumanne.
Idara hiyo imesema mshukiwa huyo amekiri kuwa alitengeneza video hiyo.
Mahakama ilisema kuwa video hiyo imeharibu sifa za watu na kusababisha hali ya kukosa imani katika familia za watu.
Upande wa mashtaka umeiomba mahakama kumnyima dhamana Mohammed ili kuruhusu kukamilika kwa uchunguzi na kupata ushauri wa kisheria kutoka kwa wizara ya sheria jimboni Kano.
Lakini mahakama ilimpa dhamana baada ya wakili wake kusema kuwa shtaka lake linaweza kupatiwa dhamana.
Kesi hiyo itasikilizwa tena tarehe 5 mwezi Februari mwaka 2021.
