Hii leo Spika wa bunge na naibu wake watachaguliwa rasmi na baadae kufuatia shughuli ya wabunge waliochaguliwa kula viapo vya utii.
Hata hivyo kuna maswali mengi yanaulizwa iwapo bunge hili ambalo asilimia zaidi ya 80 ni kutoka chama tawala cha CCM litaweza kuisimamia vyema serikali katika shughuli zake.
