Maseneta kuvaa mavazi ya kitamaduni kwenye Bunge la Seneti


Spika wa bunge la Seneti nchini Kenya amewaruhusu maseneta kuvaa nguo za kitamaduni ndani ya bunge.

Maseneta, wa kiume na wa kike, awali waliruhusiwa kuingia kwenye bunge wakiwa wamevalia mavazi rasmi au mavazi ya watoa huduma, nguo za diniau nguo nyingine kwa idhini maalumu.

Spika Ken Lusaka, akiridhia kufanyika kwa mabadiliko hayo siku ya Jumanne, alisema katiba inaruhusuwatu kudumisha utamaduni wao.

Aliulizwa kwa nini seneta kutoka jamii ya Wamasai alikuwa amevaa shuka yenye shanga nyekundu wakati kikao cha bunge.

Wajir Senator Abdulahi Ali said relaxing the rules would lead to "all manner of dressings" in parliament.

Ali Seneta wa Wajir Abdulahi Ali alisema kulegeza sheria hizo kutasababisha "mavazi ya kila aina" bungeni.

Lakini Spika Lusakaalisema haitakuwa haki kumtaka Seneta Ledama Ole Kina kuondoka bungeni kwa kuwa alikuwa na vazi la heshima.

Seneta Kina aliweka picha ya video kwenye mtandao wa twitter akionesha vazi lake.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia