Riek Machar ashutumiwa kwa “kushindwa kuongoza”


Makamu wa Rais wa Sudan Kusini, Riek Machar, ameshutumiwa kwa "kushindwa kuongoza" na afisa wa juu wa chama chake cha Sudan People's Liberation Movement in Opposition (SPLM-IO).

Katibu Mkuu Peter Tingo , amewasilisha barua ya kazi siku ya Jumanne baada ya kutumikia nafasi hoyo kwa miaka minne.

Amemshutumu bwana Machar kwa kushindwa “kuonesha utawala bora” na kukiongoza chama bila mashauriano.

Ofisi ya Machar haijasema lolote kuhusu shutuma hizo.

“Umekiendesha chama bila uwazi, hasa katika masuala ya kufanya maamuzi. Hauheshimu muundo wa taasisi uliowekwa na katiba ya taasisi,” Bw. Tingo aliandika katika barua yake ya kuacha kazi.

Amesema kuwa kuacha kwake kazi hakutaathiri utekelezaji wa makubaliano ya amani yaliyotiwa saini na Bw.Machar na hasimu wake wa kisiasa Rais Salva Kiir mwezi Februari baada ya miaka kadhaa ya mzozo.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items