Ukianza kuyaona haya, elewa hakupendi

 

Wakati mwingine huwa inatokea mtu kuwa kipofu wa macho..hajui wakati gani wa kufanya maamuzi..

Tambua tu kuna muda unafika kwenye mahusiano kuna kuwa hakuna options zaidi ya kumove on...hizo hatua zikifika usiforce kubaki move on..ndio maana tunasema ukitaka kuachana na mtu usianze kuhesabu mema ooh sijui alininunulia simu..sijui alinipeleka dubai..no angalia utu na heshima yako na thamani yako..

Yaani wewe umeshajua mtu ana mtu mwingine na unamuuliza anakiri kabisaa ninaye halafu unaanza kumwambia niambie kati ya mimi na yeye unampenda nani!!

Are u seriuos!!!ukiona hivo ujue huna muda hapo no matter how..mtu anakwmbia niko njia panda sijui nimpende nani kati ya wewe au yeye halafu bado umoo tu unalia lia tu eti niambie unampenda nani!!

Ndugu yangu weee unataka mpaka ufunuliwe na malaika ndotoni ndio ujue kuwa unahitaji kuondoka. Jiongeze hakuna furaha kuwa na mtu anayekuona kama gari, anakuendesha anavyotaka.

Kulia twende kushoto twende yaani upo upo tu kama kisiki. Fanya maamuzi magumu leo na sio kesho ujiokoe hakuna atakaekuja kukuokoa....!!!!

Post a Comment

0 Comments