Rais Recep Tayyip Erdogan amezungumza kwa njia ya simu na Rais wa Urusi Vladimir Putin.
Kulingana na taarifa kutoka kwa Wizara ya Mawasiliano ya Rais, mazungumzo hayo yamegusia uhusiano wa Uturuki na Urusi, haswa huko Nagorno-Karabakh na Syria, na kuadili maendeleo ya mkoa.
Wakati wa mkutano, Erdogan alisema kuwa hatua sahihi ilichukuliwa kama njia ya suluhisho la kudumu juu ya Nagorno-Karabakh jioni iliyopita.
ErdoÄŸan amesisitiza kuwa Armenia izingatie na kuheshimu makubaliano mapya yaliyotiwa saini.
Erdogan alisisitiza umuhimu wa kurudi nyumbani kwa watu wa Azerbaijan ambao walilazimika kuondoka Karabakh kutokana na uvamizi wa Waarmenia na kufungua barabara kati ya Azerbaijan na Nakhchivan.
Azerbaijana na Armenia zimesaini makubaliano ya kusitisha mapigano kwa ushirikiano wa Rais wa Urusi Vladimir Putin.
