Nourin Mohamed Siddig: Msoma Kurani aliyeupa mtindo wa kiafrika umaarufu

 


Nourin Mohamed Siddig aliposoma Kurani, watu duniani kote walielezea sauti yake kama yenye kujitokeza ya aina yake, mfano huzuni.


Sauti na mbinu yake ya kipekee ya kughani Kurani kulimfanya awe mmoja wa wasomaji maarufu wa Kurani duniani.


Athari zake, kifo chake akiwa na umri wa miaka 38 kupitia ajali ya gari nchini Sudan mnamo mwezi Novemba aliombolezwa kutoka nchini Pakistan hadi Marekani.


"Dunia imepoteza moja ya sauti ya kipekee kipindi hiki," aliandika ujumbe kwenye mtandao wa Twitter, Imamu Omar Suleiman kutoka Texas.


Hind Makki, msomi, raia wa Marekani mwenye asili ya Sudan alisema ni vigumu kuelezea sifa za usomaji huo.


"Kuna uhalisia wa Afrika ambao huzungumziwa hata kama hawawezi kuelewa moja kwa moja ni nini, wanakifurahia," amesema.


Kwa mujibu wa mwana historia Sylviane Diouf, sala, kukariri na kughani Kurani kwa watumwa Waislamu wa Afrika Magharibi, ambako kunaweza kusikika sawa na vile wanavyosoma Waislamu wengine wa eneo la Sahel hadi nchini Sudan na Somalia, huenda kumechangia "mtindo wa kipekee wa usomaji kwa Wamarekani wenye asili ya Afrika".


Kulingana na utamaduni, Kurani, kitabu kitakatifu kwa Waislamu, huwa kinasomwa kwa mtindo wa kama mawimbi fulani hivi, yaani kupaza na kushukisha sauti kama wimbo, jinsi ilivyokuwa ikihamasishwa Mtume Muhammad (S.A.W), aliyesema kuwa watu wanastahili "kuipendezesha Koran kwa sauti zao".


Hupendeza zaidi usomaji wa Kurani wakati idadi kubwa ya watu wanajumuika pamoja kwa ajili ya matukio ya kidini kama vile ibada wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani katika sala ya tarawehe.


Huenda kukawa na utofauti wa toni na matamshi kulingana na jiografia, utamaduni na kulingana na historia katika dunia ya Kiislamu zaidi ya Mashariki ya Kati.


Usomaji wa Kurani wa Siddiq na pia kifo chake kulileta angalizo kubwa katika mtindo wa kiafrika wa kughani Kurani.


Mtindo wake aliotumia, chanzo chake ni shule ya kitamaduni ya kujifunza kusoma Kurani kijijini mwake, al-Farajab, magharibi mwa mji mkuu wa Khartoum, katikati ya miaka ya 1990.


Na hatimaye alipohamia mji wa Khartoum, aliongoza sala katika misikiti kadhaa mjini na watu wakaanza kupenda jinsi anavyoghani Kurani.


Umaarufu wake ulisambaa pale video zake alipokuwa akisoma Kurani zilipoanza kusambazwa kwenye mtandao wa YouTube.


Wakati sauti zinaelezewa kuwa na kiwango cha noti saba ambacho ni maarufu sana Mashariki ya Kati, usomaji wa Kurani wa Siddig ulikuwa kwa mtindo wa kiwango cha noti tano ambacho ni maarufu katika maeneo ambayo idadi kubwa ya watu ni Waislamu, eneo la Sahel na pembe ya Afrika.


"Hii ndiyo toni ambayo nimekuwa nikiifahamu nilipokuwa ninakua eneo la jangwani; ni kama [muziki wa kitamaduni wa Sudan]", amesema Al-Zain Muhammad Ahmad, msomaji mwingine maarufu wa Kurani nchini Sudan.


"Wanaosoma Kurani eneo la Mashariki huzingatia mfuatano wa sauti, kama ilivyo Misri, eneo la Hijaz, Afrika Kaskazini na kwingineko."


Katika miongo ya hivi karibuni, mitindo ya kughani Kurani Mashariki ya kati imekuwa maarufu kwenye maeneo mengi ya Afrika na kote duniani hasa maeneo ya mijini.


Wasikilizaji wa Koran wamekuwa wakifikia rekodi zilizopo, matangazo ya redio kupitia masafu mafupi, kaseti, CD zilizorekodiwa na kusambazwa au kuuzwa na mashirika kutoka Misri na Saudi Arabia.


Wanafunzi wanaorejea kutoka chuo kikuu cha Al-Azhar cha Misri na chuo kikuu cha Kiislamu cha Medina, pamoja na michango kutoka kwa mashirika ya maeneo ya ghuba, kumesaidia kusambaa kwa umaarufu wa mtindo wa kughani Kurani wa Mashariki ya Kati ikiwemo eneo la Afrika huku wengine hata wakifanya vizuri zaidi katika usomaji wa Kurani.


Lakini intaneti na mitandao ya kijamii kumebadilisha mambo hasa kutoka kizazi kichanga hadi sauti zilizozoeleka.


Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi