Waziri Mkuu wa Algeria awasilisha barua ya kujiuzulu

Waziri Mkuu wa Algeria Abdelaziz Djerad, aliwasilisha barua ya kujiuzulu kwake kwa Rais Abdelmadjid Tebboune baada ya matokeo rasmi ya uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 12 Juni kutangazwa.

Katika taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Rais, ilielezwa kuwa Tebboune alimpokea Waziri Mkuu Djerad kwenye ikulu ya Rais katika mji mkuu.

Taarifa hiyo ilibainisha kuwa Djerad alipeleka barua yake ya kujiuzulu kwa Rais baada ya matokeo rasmi ya uchaguzi kutangazwa.

Ilielezwa kuwa ombi la kujiuzulu kwa Djerad lilikubaliwa, ingawa ataendelea kuhudumu kwenye wadhifa wake hadi serikali mpya itakapoundwa.

Iliarifiwa kuwa Tebboune alimshukuru Djerad kwa kufanikisha na kutekeleza majukumu yake wakati wa kipindi kigumu kama vile janga la corona (Covid-19).

Kulingana na matokeo rasmi ya uchaguzi mkuu uliofanyika Algeria mnamo Juni 12, Chama cha Ukombozi cha Kitaifa (FLN) kilikuwa chama cha kwanza kikiwa na viti 98. Katika Bunge lenye viti 407, vyama vya kujitegemea vilishinda viti 84, Harakati ya Jamii ya Amani ya Kiislam viti 65, Democratic National Union (RND) viti 58, Future Party viti 48, National Building Movement viti 39, na Justice and Development Front Party viti 2.

 

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items