OFISA Habari wa Simba, Haji Manara amebwaga manyanga ndani ya Simba na kwa sasa nafasi yake inachukuliwa na Ezekiel Kamwaga ambaye anakuwa Kaimu Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Klabu kwa kipindi cha miezi miwili.
Taarifa
rasmi ambayo imetolewa na Simba kupitia ukurasa wao wa Instagram
imeeleza kuwa Bodi ya Wakurugenzi ya Klabu ya Simba, kwa kauli moja
imeridhia matakwa ya ndugu Haji Manara ya kutoendelea kuhudumu katika
nafasi ya msemaji wa Klabu ya Simba.
Bodi
inamshukuru kwa maneno aliyoyatumia kuwaaga wana Simba katika kundi la
viongozi wa Simba, (Simba HQ) na kwa kazi aliyoifanyia Klabu ya Simba
katika kipindi alichoshika nafasi hiyo na inamtakia heri katika shughuli
zake.
0 Comments