https://monetag.com/?ref_id=TTIb Mwanamke mweusi ashinda taji la malkia wa urembo Ireland | Muungwana BLOG

Mwanamke mweusi ashinda taji la malkia wa urembo Ireland



"Ni furaha kuwa sura ambayo wasichana wadogo weusi wanaweza kujivunia na kusema amefanya hivyo hata sisi tunaweza.'"

Hayo ni maneno ya msichana mwenye umri wa miaka 26 anayesomea matibabu Pamela Uba. Amevishwa taji la malkia wa urembo nchini Ireland mwaka 2021, na kuwa mwanamke wa kwanza mweusi kushinda taji hilo.

Mashindano hayo yamekuwa yakifanyika tangu 1947, lakini Pamela anasema kwamba inashangaza kwamba miaka 74 ilipita bila mtu tofauti kushinda taji hilo.

‘’Mimi ni wa kwanza na ni furaha – watu wananitegemeana sikufikiria nitapata fursa hii’’.

Pamela alielekea katika taifa la Jamuhuri ya Ireland kutoka kusini mwa Africa akiwa na umri wa miaka saba pamoja na mamake na ndugu zake watatu.

 

Post a Comment

0 Comments