Kamati inayochunguza sera ya corona ya Bolsonaro kuwasilisha ripoti yake Brazil


Kamati ya Bunge la Brazil iliyoundwa kuchunguza sera ya virusi vya corona ya serikali ya rais Jair Bolsonaro itawasilisha ripoti yake leo baada ya kufanya kazi kwa muda miezi sita. 
 
Baraza la Seneti limesema Seneta Renan Calheiros atawasilisha ripoti hiyo inayosubiriwa kwa hamu na umma wa Brazil, taifa ambalo lilishuhudia madhara makubwa ya janga la virusi vya corona.
 
 Rasimu ya ripoti hiyo ambayo tayari imesambaa miongoni mwa vyoimbo vya habari vya Brazil inapendekeza miongoni mwa mwambo mengine, kuwajibishwa kwa watu 70 na kampuni mbili pamoja na kushtakiwa kwa rais Bolsonaro kwa madai ya kutenda makosa 11 ya uhalifu. 
 
Kulingana na ripoti za vyombo vya habari, maseneta walijadili maudhui ya mwisho ya ripoti hiyo hadi usiku wa manane na kuamua kuondoa tuhuma mbili kutoka orodha hiyo. 
 
Kamati hiyo ilianza kazi yake mwezi Aprili, kwa dhima ya kuchunguza makosa yaliyotendwa na serikali ya rais Bolsonaro katika kushughulikia kadhia ya janga la Corona.

 

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items