Watoto wachanga walizaliwa na aina ya HIV sugu kwa dawa kabla ya matibabu-WHO

 


Shirika la Afya Ulimwenguni limesema kuwa karibu nusu (asilimia 45) ya watoto wachanga waliozaliwa katika nchi kumi za Afrika walizaliwa na aina ya HIV ambayo ni sugu kwa dawa inayotumika hata kabla ya kuanza matibabu.


Wataalam wana wasiwasi kuwa takwimu zinaweza kuwa za juu zaidi.


WHO inasema watu milioni 25.4 wanaishi na virusi vya ukimwi barani Afrika.


Ni Nigeria, Cameroon, Togo, Afrika Kusini, Uganda, Kenya, Malawi, Msumbiji, Zimbabwe na Eswatini pekee ndizo zimefanya tafiti zinazoangalia ukinzani wa dawa za HIV kabla ya matibabu.


Hii hugunduliwa kwa watu ambao hawana historia ya kutumia dawa za HIV kabisa.


Nchi nyingine za Kiafrika hazijaweza kufanya tafiti za kina kuhusu hili.


WHO inasema watoto wanaozaliwa na virusi vya ukimwi wanaweza kuwa ni matokeo ya wanawake wajawazito kutopimwa mara kwa mara na wengine kutokunywa dawa zao mara kwa mara.


Dk Fausta Moesha kutoka ofisi ya WHO kanda ya Afrika anasema matokeo haya yanaangazia haja ya nchi kununua na kuwapa watoto dawa inayojulikana kama Dolutegravir.


Matibabu haya yametajwa kuwa ya mabadiliko kutokana na ufanisi wake na ni rahisi kwa matumizi.


Ni nchi chache tu barani Afrika ambazo zimesambaza dawa hii hadi sasa.

Post a Comment

0 Comments