Kuna 'uwezekano mkubwa' mateka walikuwa katika hospitali ya Al-Shifa - Netanyahu


 Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anasema kuna "uwezekano mkubwa" kwamba mateka wanaoshikiliwa na Hamas walikuwa katika hospitali ya Al-Shifa mjini Gaza.


Ilikuwa "sababu mojawapo iliyotufanya tuingie hospitalini", anasema katika mahojiano na CBS Evening News.


Israel imewashutumu Hamas mara kwa mara kwa kuwa na kambi kubwa chini ya Al-Shifa - jambo ambalo Hamas inakanusha.


Vikosi vya Israel vilivamia hospitali ya Al Shifa siku ya Jumatano, lakini Netanyahu anasema walipofika, mateka hawakuwapo tena.


"Kama walikuwa [huko], walitolewa nje," anasema. Anasema serikali yake ina "intelijensia kuhusu mateka," lakini anaongeza "kadiri ninavyosema kidogo juu yake, bora zaidi".

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items