UWT Babati Mjini wapongeza jitihada za Rais Samia kuboresha Sekta Afya.

 


Na John Walter-Manyara

Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) mjini Babati imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha kuboresha Sekta ya afya ili wananchi wapate huduma bora.

Kauli hiyo imetolewa na  Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT)  mjini Babati Eva Luoga baada ya kufanya ziara katika Hospitali ya Halmashauri ya mji wa Babati kutembelea wagonjwa katika wodi ya wanawake na kutoa misaada mbalimbali.

UWT Babati mjini wamejionea  wodi mpya ya kisasa ya kinamama na watoto iliyosaidia kuondoa changamoto ya wanawake kushirikiana kitanda wanapofika kupata huduma.

Jumuiya hiyo imeadhimisha mwaka mmoja tangu kuchaguliwa kwa Mwenyekiti wao wa taifa Marry chatanda na Makamu wake  Zainabu shomari.

Luoga ameeleza kuwa wametembea  wodi ya wazazi kuwafariji wanawake wenzao waliojifungua, wajawazito na watoto njiti na kuridhishwa na huduma zinazotolewa hospitalini hapo.


Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items