Shirika la ndege la Ethiopia nchini Nigeria limepiga marufuku mikoba iliyopewa jina la utani "Ghana Must Go" kutoka kwa safari zao za ndege huko.
Mizigo hiyo ilipata jina la utani nchini Nigeria katika miaka ya 1980, wakati maelfu ya wahamiaji wasio na vibali, wengi wao wakiwa Waghana, walifukuzwa.
Watu walikimbia na mifuko iliyokaguliwa ya rangi nyekundu na bluu migongoni mwao.
Sasa, shirika la ndege linasema, wabebaji wa mifuko hiyo, inayopendwa na wafanyabiashara, inaweza kuathiri vibaya vifaa vya uwanja wa ndege.
Katika taarifa yake Shirika la Ndege la Ethiopia lilisema marufuku hiyo ilianzishwa kwa sababu ya "kutokea mara kwa mara kwa uharibifu wa mikanda ya kusafirisha mizigo katika viwanja mbalimbali vya ndege, na kusababisha gharama kubwa kwa mashirika ya ndege husika".
Mifuko hiyo inaweza kutumika ikiwa "ingepakiwa vya kutosha kwenye katoni au kontena gumu la mstatili".
Ethiopia Airlines hufanya safari za ndani na kikanda nje ya kitovu cha kibiashara cha Nigeria, Lagos.
Mifuko hiyo ni maarufu sana kote barani Afrika, na sehemu kubwa ya dunia, na inaweza kuonekana katika viwanja vya ndege vingi.
Pia ina majina tofauti. Nchini Kenya, kwa mfano, inajulikana kama mifuko ya Nigeria, nchini Tanzania inajulikana kwa jina Shangazi kaja na Wazimbabwe wanaiita mifuko ya Botswana.
Mnamo mwaka wa 2017 KLM na Air France, waliweka marufuku kwa sababu walisema mifuko hiyo inaweza kutanua na kuziba mifumo ya utoaji mizigo.
