F Waliohitimu kidato cha sita 2025 watakiwa kuripoti kupata mafunzo ya JKT | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Waliohitimu kidato cha sita 2025 watakiwa kuripoti kupata mafunzo ya JKT

 


Jeshi la Kujenga Taifa JKT limewataka vijana waliohitimu kidato cha sita mwaka 2025 kutoka shule mbalimbali hapa nchini kujiunga na mafunzo ya jeshi hilo kwa mujibu wa sheria ambapo wanatakiwa kuanza kuripoti kuanzi kesho mei 28, hadi Juni 8 mwaka huu.

Amesema orodha ya vijana ya vijana waliochaguliwa kujiunga na mafunzo hayo inapatikana kwenye tovuti ya JKT ya www.jkt.mil.tz ambapo watapata orodha kamili na mahali walipopangiwa na vitu wanavyotakiwa kuwa navyo wakati wa kujiunga.

Akizungunza na waandishi wa Habari leo Mei 27, 2025 Jijini Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT. Meja Jenerali Rajabu Mabele, Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala wa JKT, Kanali Juma Mray amezitaja baadhi ya kambi ambazo vijana hao wanatakiwa kuripoti huku wakiwa na vifaa ni pamoja na vifaa vinavyohitajika.

Kanali Mray amefafanua zaidi ya kuwa kwa vijana wenye ulemavu wa kuona kwa macho wanapaswa kuripoti katika kambi ya ruvu ilioko mkoani pwani kwa ndio kambi yenye miondombinu ya kuwawezesha kupata mafunzo.

Kanali mray amesisitiza kuwa nafasi hizo zinatolewa bure na zinapatikana katika tovuti ambayo imeainishwa na JKT huku akiwasisitiza wanafunzi waliohitimu kidato cha sita mwaka huu na jamii kwa ujumla wasikubali kurubuniwa kuhusu nafasi hizo.

Kanali Mray ametaja baadhi ya vifaa ambavyo wanapaswa kuripoti navyo kuwa ni bukta ya rangi ya 'dark blue' yenye mpira kiunoni(plastic), iliyo na mfuko mmoja nyuma, urefu unaoishia magotini, isiyo na zipu, track suit ya rangi ya kijani au blue, nataka zote zinazohitajika katika udahili wa kujiunga na elimu ya juu, zikiwemo cheti cha kuzaliwa,.

Amesema ili kufahamu kambi ambayo kijana aliyopangiwa atatakiwa kuingiza jina la shule au namba ya shule aliyohitimu elimu ya kidato cha sita ndipo atapata orodha kamili ya majina hayo.

Post a Comment

0 Comments