Na John Walter-Babati
Halmashauri ya Kijiji cha Magugu imependekeza kupandisha bei ya vibanda 83 vya serikali kutoka shilingi 5,000 hadi shilingi 30,000, sawa na ongezeko la asilimia 500.
Mpango huu unatarajiwa kuongeza mapato ya kijiji hadi shilingi
milioni 51 kwa mwaka.
Mwenyekiti wa Kijiji, Loya Amos, amesema ongezeko la
bei limechukuliwa kutokana na kuongezeka kwa gharama za maisha, hivyo ni
vyema kuhakikisha vibanda vinapandishwa bei ili kijiji kiendelee kutoa huduma
na kusimamia miradi ya maendeleo.
Diwani wa Kata ya Magugu, Stanley Charles,
amewashauri uongozi wa kijiji kuhakikisha wananchi wanashirikishwa kwa
usahihi kuhusu mapato na matumizi ya vibanda hivyo.
Amesema endapo mapato yatadhibitiwa vizuri, maendeleo ya
kijiji yataimarika, michango ya wananchi itapungua, na malalamiko yatapunguzwa.
Diwani Stanley ameongeza kuwa ongezeko hili halihusishi
vibanda vya wajasiriamali wa sokoni, bali ni kwa vibanda vya serikali
vinavyosimamiwa na kijiji.
Uamuzi huu unalenga kuboresha usimamizi wa mapato na
kuhakikisha maendeleo ya kijiji yanaendelea kwa uwazi na uwajibikaji.
0 Maoni