Kumekuwa na uvumi kuwa, winga wa Yanga mbrazil Andrey
Coutinho huenda akatimka kunako klabu ya hiyo na tayari kuna timu inamuwania
ili kuinasa saini yake. Katibu mkuu wa Yanga Dkt. Jonas Tiboroha amesema , wao kama uongozi bado hawajapokea taarifa rasmi kutoka
klabu yoyote ikionesha nia ya kumtaka
mchezaji huyo.
”Hatujapata document
timu kutoka timu yoyote inayomtaka Coutinho kwenda kufanya majaribio au
kumsajili jumla, lakini lisemwalo lipo bwana, huwezi kujua mara nyingi maajenti
wanapitia kwa watu kabla ya kufika kwetu. Hata taarifa za Kpah Sherman zimekuja
muda si mrefu lakini watu waliulizia kwa muda mrefu sana”, amesema
Tiboroha.
Andrey Coutinho amekuwa akisugua benchi tangu alipopata
majeraha ya muda mrefu kwenye msimu wa ligi uliomalizika na tangu arejee
uwanjani amekuwa hapati nafasi ya kucheza mara kwa mara kwa mara kwenye kikosi
cha kwanza.
Ujio wa Deus Kaseke kutoka Mbeya City
pamoja na Godfrey Mwashiuya kutoka Kimondo umezidi kufuta ndoto za mbrazil huyo
kuendelea kupata nafasi ya kucheza kwenye kikosi cha Yanga kutokana na wawili
hao kuonesha kiwango ambacho kimekuwa kikimvutia kocha mkuu wa timu hiyo Hans
van Pluijm.
Coutinho alisajiwa Yanga na aliyekuwa kocha wa timu hiyo
mbrazil Marcio Maximo na alionesha kiwango cha juu kwenye mechi zake za
mwanzoni kabla ya kukubwa na majeraha yaliyomuweka nje kwa muda mrefu.