Dr. SLAA Sina Mpango wa Kuhama CHADEMA

HABARI ZA HIVI PUNDE: "HAKUNA SINTOFAHAMU YOYOTE KATI YA YANGU MIMI Dr. Slaa, Mbowe, Mnyika, Tundulisu na wengineo kwa ujio wa mgeni Mhe. Lowassa wala hakuna chochote kilichoharibika ndani ya CHADEMA, NCCR, NLD, CUF wala kwa wanachama, wafuasi na wapenzi wa UKAWA.

Myaonayo na myasikiayo kwenye mitandao ya kijamii ni kauli za wafa maji. Tulichokifanya UKAWA ni kuunganisha dhamira zetu pamoja. Narudia tena; tulichokifanya kama UKAWA ni kuunganisha dhamira zetu pamoja.

Zaidi sana napenda kusisitiza jambo hili kwa umma kwamba NDANI YA VYAMA VINAVYOUNDA UKAWA HAKUNA MWENYE DHAMANA WALA MAMLAKA YA JUU ZAIDI YA MWINGINE HATA KWA KWA YULE MSHABIKI"

By. Dr. Wilbroad Slaa (katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo-CHADEMA)

Chanzo: Radio One