Matamshi ya Rais Barack Obama wa Marekani kuhusu umuhimu wa
kuimarishwa demokrasia katika nchi za bara la Afrika, yamekabiliwa na radiamali
kali kutoka kwa baadhi ya viongozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Lambert Mendé, Msemaji na Waziri wa Mawasiliano wa nchi hiyo
amesema kuwa, matamshi ya kiongozi huyo wa Marekani juu ya suala la demokrasia
ni jambo ambalo viongozi wengi wa Magharibi wamekuwa wakilihitajia kwa miaka
mingi. Amesema kuwa, Rais Obama anataka kuonyesha kwamba, ni nchi pekee za
Kiafrika ambazo zinatakiwa kusoma na kujifunza demokrasia na kupambana na
ufisadi na kwamba suala hilo pekee ndilo
litakalomaliza matatizo ya nchi za bara hilo .
Kwa upande wake Jean-Didier Elongo, mmoja wa viongozi wa
chama tawala nchini Kongo DR, amesema kuwa, rais huyo wa Marekani kwanza haijui
hali halisi ya nchi za Kiafrika, suala ambalo limemfanya kutoa maneno hayo bila
kuzingatia. Amesema kuwa, Rais Barack Obama anamaliza muda wake wa urais nchini
Marekani huku akiwa hata helewi uhalisia wa hali ya Afrika ambayo ana mahusiano
nayo, hivyo katika hali kama hiyo hakutarajiwi
kheri yoyote kutoka kwake.
Akihutubia mkutano wa viongozi wa nchi za Afrika mjini Addis Ababa , Ethiopia Rais
Obama alisisitizia umuhimu wa kuimarishwa demokrasia na kupambana na ufisadi
barani Afrika.