Magaidi watatu wa kundi la kitakfiri la Al-Shabab wameuawa
nchini Kenya
katika Kaunti ya Lamu kufuatia mapigano na Jeshi la Ulinzi la Kenya KDF.
Msemaji wa KDF Kanali David Obonyo amesema wanajeshi watano
wamejeruhiwa katika mapigano hayo yaliyojiri karibu na eneo la Basuba, Lamu leo
asubuhi saa nne.
Ameongeza kuwa wanajeshi wamefanikiwa kunasa bunduki mbili
aina ya AK-47 na risasi kadhaa. Kanali Obonyo amesema gari la KDF lililengwa
kwa bomu la kienyeji yapata kilomita saba kutoka Basuba na hapo wanajeshi
waliokuwa wakilinda doria wakafyatuliana risasi na magaidi na kuwaua watatu
kati yao .
Amesema magaidi kadhaa wakifanikiwa kutoroka wakiwa na
majeraha. Wakaazi wa eneo hilo wamesema
walisikia milio ya risasi na kuona moshi ukitoka katika Msitu wa Boni eneo
ambalo jeshi la Kenya
sasa linatekeleza oparesheni kali kuwatimua magaidi al-Shabab.